Mkurugenzi wa Trickster, Sonobe Atsushi akizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani) jijini Dar es Salaam leo, kuhusiana na uzinduzi wa shindano la kibiashara ambali litakuwa katika nchi tano za Afrika.
Meneja Mradi kutoka kampuni ya Afrika New Business Development Department(DMM)  Bw.Alex Kapungu  akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi wa Trickster, Sonobe Atsushi.


KAMPUNI ya Kijapani inayofanya shughuli zake nchini (Tricster)  imeandaa shindano la wazo la biashara  litakalozishirikisha  nchi tano  za Afrika zikiwemo Kenya,Rwanda,Zambia,Zimbabwe na Tanzania mwenyeji wa  mashindano hayo kwa mwaka 2016.


Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Meneja Mradi kutoka kampuni ya Afrika New Business Development Department(DMM)  Bw.Alex Kapungu ambao ndio  wadhamini wa shindano hilo ameeleza kuwa lengo la shindano hilo ni  kusaidia kuboresha ujasiriamali katika bara la Afrika.


“Shindano hili linafanyika kwa mara ya kwanza na hivyo ni fursa nzuri kwa wajasiriamali na wale wanaotaka kuwa wajasiriamali kushiriki na baadaye kufanikisha wazo hilo kiutendaji kwa kuwa biashara halisi”alisema Bw.Alex.


Aidha ameongeza kuwa vigezo vya kushiriki shindano hilo ni mshiriki awe amefikisha miaka 18 na kuendelea, awe anajua kuongea na kuandika lugha ya kiingereza na kuwa na hati ya kusafiria.


Naye Mkurugenzi wa Trickster Bw.Sonobe Atsushi amesema washindi watakaoingia nusu fainali watapata fursa  ya kutembelea nchi ya japani ambapo mshindi wa kwanza atapata fedha taslimu  Dola elfu tano za kimarekani.


Pia ametoa wito kwa watanzania kujitokeza na kushiriki kwa wingi ili wapate fursa ya kuanzisha biashara kupitia mawazo watakayoyatoa na hivyo kupanua wigo wa biashara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...